|
Historia ya kwaya Bandeko
Kikundi hiki kilizaliwa katika Milano kutokana na mang’amuzi ya baadhi ya vijana waliokuwa wamekwenda
Afrika na Amerika ya kusini kufanya kazi za kujitolea. Mpango huu ulikuwa
umepangwa na kikundi cha “Africa Oggi” – Afrika Leo.
Kwenye miaka ya mwanzo ya tisini ('92/'93), kikundi
cha vijana wapato kumi walikuwa wanakusanyika kwa ajili ya kuandaa na
kuimba nyimbo za misa takatifu. Huu ulikuwa wakati mahususi sana wa kuwakutanisha
na kuwaunganisha vijana wa “Africa Oggi”. Nyimbo hizi za lugha
ya kigeni zimekuwa kama chombo cha kusaidia kuishi maisha ya kiroho, na
vilevile kushirikisha waumini zaidi katika sadaka ya misa takatifu.
Siku moja, vijana wawili (wanachama wa
Bandeko) walitaka kufunga ndoa yao kanisani. Hivyo basi waliwaomba kwaya
ya Bandeko waimbe wakati wa misa ya ndoa yao (Monza 03/09/1993). Tangu wakati huo, kikundi
cha kwaya ya Bandeko walianza kupapa mialiko katika Parokia mbalimbali
kwa ajili ya kwenda kuimba wakati wa ibada za misa za kimisionari. Kwa
kweli lilikuwa wazo zuri sana kuwajibika namna hii kwani ilikuwa njia
mojawapo ya kukusanya sadaka/msaada wa pesa ambao ulisaidia miradi mbalimbali
ya mshikamano na misioni.
Kwenye mwaka wa 1996, kwaya ilijichagulia jina la Bandeko.
Kutoka wakati huo, kwaya yetu ilizidi kujulikana
sana kiasi kwamba tulianza kupata mialiko mbalimbali kama vile: sikukuu
za halaiki, sherehe za ubatizo, siku za kimisionari, katika mihadhara
mbalimbali na maandamano ya amani, na sherehe nyingine nyingi.
Mpaka siku hizi bado tunaendelea kujifunza nyimbo mpya. Tunafanya mazoezi
ya nyimbo mpya na za zamani mara moja kwa wiki.
|