|
Mpaka kuweza kufanikisha huu mtandao
haikuwa kazi rasisi. Hata hivyo, hilo siyo tatizo, muhimu ni kwamba tumefanikiwa.
Wazo hili lilikuwepo tangu mwaka wa 1999
(elfu moja mia tisa na tisini na tisa): baada ya subira nyingi tulifanikiwa
kusahihisha maneno/maandishi ya baadhi ya nyimbo ambazo wanakwaya wetu
(wa zamani na wapya) wangependa kutushirikisha. Shukrani za dhati ziwaendee
wale wanakwaya wote walioshiriki katika kusanii nyimbo hizi.
Shukrani nyingi sana zimwendee Davide
na Vincenzo kwa kazi kubwa ya ufundi na ustadi aliyofanya
ya kubuni huu mtandao. Asante, umefanya kazi nzuri sana. Nakushukuru hata
kwa saburi nyingi uliyokuwa nayo katika kutafsiri maoni yangu. Nina imani
kuwa kazi hii ya kutayarisha huu mtandao itakuletea sifa na umaarufu mwingi
ndani ya Bandeko.
Shukrani nyingine ziwaendee wafuatao:
Paolo (Pauli) kwa tafsiri katika lugha ya Kihispania.
Kazi yako imeboresha nakala yetu katika lugha ya Kiitaliano.
Padri Salutaris, mmisionari wa shirika la Waconsolata,
kwa tafsiri katika lugha ya Kiswahili, kitu ambacho, kwa namna ya pekee
nijivunia kwa sababu inatuwezesha kurusha hewani mang’amuzi yetu
katika lugha ambayo imeenea sana katika bara la Afrika, ambayo kwayo wengi
wetu tunaitumia. Tunawashukuru wote wawili, ninyi na ndugu zetu kabisa.
Tunatumaini kwamba, mtandao
huu hautakuwa tu chombo cha kutoa ushuhuda wa mang’amuzi mbalimbali,
bali utakuwa ishara ya amani na umoja kwa wale wote ambao watautembelea.
Carlo
|